Wednesday, 20 May 2015

Watinga kuchukua maiti wakivalia nguo za magunia




Ndugu na jamaa wa marehemu Victoria Silvester (53), wakiwa ndani ya chumba cha kuhifadhia maiti cha Hospitali ya Rufaa ya KCMC, huku wakiwa wamevaa magunia walipokwenda kuuchukua mwili kwa ajili ya mazishi, mkoani Kilimanjaro jana. Picha na Dionis Nyato 


Posted  Jumatano,Mei20  2015  saa 9:14 AM
KWA UFUPI
  • Walikuwa wamevalia magunia, lakini sababu ya kuvalia nguo hizo haikuwa kama maandiko hayo yanavyosema kuwa “kwa sababu hiyo jifungeni nguo za magunia; ombolezeni na kulia kwa uchungu; kwa maana hasira kali ya Bwana haikugeuka na kutuacha”.
SHARE THIS STORY
 
 
 
0
Share
Moshi. Ilikuwa ni kama kutekeleza maandiko ya Biblia yanayosema “jifungeni nguo za magunia, ombolezeni na kulia kwa uchungu”, wakati ndugu walipokwenda Hospitali ya Rufaa ya KCMC kuchukua mwili wa marehemu.
Walikuwa wamevalia magunia, lakini sababu ya kuvalia nguo hizo haikuwa kama maandiko hayo yanavyosema kuwa “kwa sababu hiyo jifungeni nguo za magunia; ombolezeni na kulia kwa uchungu; kwa maana hasira kali ya Bwana haikugeuka na kutuacha”.
“Tumejiuliza maswali mengi, tumeshindwa kupata majibu. Tumejiuliza tuvae nguo gani hatukupata majibu. Kwa kuvaa hivi tunataka hao wauaji wajue damu hii itawalilia popote walipo,” alisema Beata Kiria, ambaye ni dada wa Victoria Sylvester aliyeuawa na watu wasiojulikana na mwili wake kuzikwa nusu kiwiliwili.
Beata na ndugu zake walifika kwenye hospitali hiyo kwa ajili ya kuuchukua mwili huo wakiwa wamevalia magunia.
Tukio hilo lilitokea jana kati ya saa 4:30 asubuhi na saa 6:00 mchana wakati ndugu hao walipofika chumba cha kuhifadhi maiti cha hospitali, huku baadhi yao wakiwa pekupeku na kusababisha watu wengi waliokuwa eneo hilo pamoja na watumishi wa hospitali kuwashangaa.
Wakiwa ndani ya chumba cha kuhifadhia maiti, ndugu hao walilia wakipaza sauti wakitaka wauaji wa mwanamke huyo wakamatwe kabla ya kuchukua mwili na kuondoka nao.
Victoria (53), mkazi wa Kijiji cha Masherini, Umbwe eneo la Kibosho aliuawa kwa kukatwa mapanga usiku wa kuamkia Ijumaa iliyopita na baadaye wauaji kuuzika mwili wake nusu na kuacha kiwiliwili nje ya nyumba waliyokuwa wakiishi, jambo lililoibua utata mkubwa ndani ya familia hiyo.
Akizungumza na gazeti hili, Kiria alisema walichagua mavazi hayo baada ya kukosa vazi lingine.
“Tulitafakari tuvae nguo gani ili kumuenzi marehemu lakini hatukupata jibu, ndiyo tukaamua tuvae magunia kuonyesha kuwa waliomuua ndugu yetu thamani yao inafanana na magunia haya,” alisema Kiria.
Imezoeleka misiba mingi ndugu huvaa suti nyeusi kwa wanaume huku wanawake wakivalia mavazi meusi au meupe ambayo baadaye hujifunika na vitambaa vyeusi au vyeupe kwa akina mama.
Kiria, ambaye alizungumza kwa niaba ya familia, alilitaka Jeshi la Polisi kuhakikisha linawatafuta na kuwakamata watu waliohusika na mauaji hayo.
Kamanda wa polisi mkoani Kilimanjaro, Fulgence Ngonyani alisema wanamshikilia mume wa marehemu, Silvester Mmasi na mtumishi wao ambaye hakumtaja kwa ajili ya mahojiano kuhusu mauaji hayo na polisi inaendelea kuwatafuta washukiwa wengine.

Watoto wa vigogo BoT wana kesi ya kujibu


SHARE BOOKMARKPRINTEMAILRATING


SHARE THIS STORY
 
 
 
0
Share
Dar es Salaam. Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu imewaona wafanyakazi wanane wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT) wanaokabiliwa na tuhuma za kughushi vyeti na kutoa hati za uongo wana kesi ya kujibu.
Uamuzi huo ulitolewa jana na Hakimu Mkazi, Nyigulile Mwaseba baada ya kupitia ushahidi uliotolewa na mashahidi wanane wa upande wa mashtaka pamoja na vielelezo vilivyowasilishwa mahakamani hapo.
Baada ya Hakimu Mwaseba kutoa uamuzi huo, alisema Juni 17 na 18, 2015, washtakiwa hao ambao wanadaiwa kuwa ni watoto wa vigogo wa Serikali wataanza kutoa ushahidi wa utetezi dhidi ya mashtaka yanayowakabili.
Wafanyakazi hao ni Justina Mungai, Christina Ntemi, Siamini Kombakono, Janeth Mahenge, Beatha Massawe, Jacquiline Juma, Philimina Mutagurwa na Amina Mwinchumu.
Washtakiwa hao kwa pamoja wanadaiwa kughushi vyeti vya kuhitimu kidato cha nne na kutoa hati za uongo kwa mwajiri wao, BoT.
Washtakiwa Mungai, Massawe na Mwinchumu, wanadaiwa kughushi vyeti hivyo mwaka 2001, wakati Ntemi, Kombakono, Mahenge na Mutagurwa wanadaiwa kughushi vyeti hivyo mwaka 2002.
Wanadaiwa kughushi vyeti vya kuhitimu kidato cha nne na kutoa BoT hati za uongo wakionyesha kuwa vimetolewa na Baraza la Mitihani la Taifa wakati siyo kweli. Washtakiwa hao ambao awali waliyakana mashtaka, wako nje kwa dhamana.

Aliyemtumia meseji Rais JAKAYA MRISHO KIKWETE hakustahili kusimamishwa-Wizara


SHARE BOOKMARKPRINTEMAILRATING
Na Suzan Mwillo, Mwananchi 

Posted  Jumatano,Mei20  2015  saa 11:31 AM
KWA UFUPI
  • Mhumba alisimamishwa kazi Mei 5, mwaka huu kwa madai ya kutuma ‘meseji’ kwa Rais Jakaya Kikwete akimweleza kuhusu ubadhirifu katika hospitali hiyo.
SHARE THIS STORY
 
 
 
0
Share
Dar es Salaam. Katibu Mkuu Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii, Dk Donan Mmbando amesema hatua iliyochukuliwa na uongozi wa KCMC ya kumsimamisha kazi mtumishi wa Idara ya Uhasibu, Paul Mhumba siyo sahihi.
Mhumba alisimamishwa kazi Mei 5, mwaka huu kwa madai ya kutuma ‘meseji’ kwa Rais Jakaya Kikwete akimweleza kuhusu ubadhirifu katika hospitali hiyo.
Hatua ya uongozi wa KCMC kumsimamisha kazi mtumishi huyo imeendelea kuibua maswali kwa watu wa kada mbalimbali kwamba imekuwaje ujumbe wa siri aliotumiwa Rais umeifikia taasisi hiyo pamoja na namba ya mtumiaji.
Wakati sintofahamu hiyo ikiendelea, Mhumba ambaye pia ni Mwenyekiti wa Chama Wafanyakazi wa Serikali Kuu na Afya (Tughe), Tawi la KCMC katika barua yake ya Mei 16 kwa Dk Mmbando, alimwomba afike kwa uongozi huo kutoa ushahidi.
Alimtaka awe shahidi wake baada ya uongozi huo kudai kuwa yeye ndiye aliyewapa ujumbe huo na namba ya mtumaji.
Hata hivyo, jana Dk Mmbando hakueleza chochote juu ya madai ya kuhusika na kutuma ujumbe huo kwa ‘meseji’ lakini alikosoa hatua iliyochukuliwa na uongozi wa KCMC kwa mtumishi huyo.
“Siyo sahihi kwa hatua waliyochukua KCMC. Kiongozi anapopewa taarifa zenye mapungufu kwenye taasisi ni kwa ajili ya kumsaidia kutatua changamoto hizo,” alisema Dk Mmbando.
Kuhusu uongozi wa hospitali hiyo kumtaka Mhumba kupeleka ushahidi wake katika kikao cha mwisho cha kamati ya nidhamu kitakachokutana Mei 26 kujadili suala hilo, Dk Mmbando alisema: “Wasiliana na uongozi wa KCMC. Hilo ni suala la kiutawala walishughulikie wao,” alisema Dk Mmbando ambaye aliwahi kuwa Mganga Mkuu wa Serikali.
Kauli ya Dk Mmbando inaendana na kauli ya Katibu Mkuu wa Tughe Mkoa wa Kilimanjaro, Simon Msuya ambaye juzi alisema uongozi huo ulitakiwa kukanusha tuhuma badala ya kumtafuta aliyetuma ujumbe.
Hata hivyo, uongozi wa KCMC umeendelea kukaa kimya hata baada ya kupelekewa maswali na gazeti hili kwa maandishi kama ilivyoelekezwa na ofisa uhusiano wa hospitali hiyo.

Wabunge wa Ukawa waikalia kooni Ikulu


SHARE BOOKMARKPRINTEMAILRATING

Mbunge wa Muhambwe, Felix Mkosamali (kushoto) akichangia bungeni mjadala wa kupitisha bajeti ya Ofisi ya Rais , Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Utawara Bora na Uhusianao na Uratibu kwa mwaka wa fedha 2015/2016, mjini Dodoma jana. Picha na Emmanuel Herman 
Na Fidelis Butahe na Sharon Sauwa, Mwananchi

Posted  Jumanne,Mei19  2015  saa 8:25 AM
KWA UFUPI
  • Mawaziri hao jana walitakiwa kueleza sababu za ofisi hiyo kushindwa kutokomeza rushwa, mikakati ya Serikali kuiwezesha Takukuru na kuipa meno ya kuwashtaki moja kwa moja watuhumiwa wa rushwa.
SHARE THIS STORY
 
 
 
0
Share
RELATED STORIES
Dodoma. Mjadala wa bajeti mwaka 2015/16 umegeuka mwiba mchungu kwa Ofisi ya Rais baada ya mawaziri watatu waliopo katika ofisi hiyo kubanwa na wabunge wa upinzani hasa wale wanaounda Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa), wakisema “njaa imeanzia Ikulu na Ofisi ya Rais inayosimamia Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) haina utashi wa kupambana na rushwa.”
Mawaziri hao jana walitakiwa kueleza sababu za ofisi hiyo kushindwa kutokomeza rushwa, mikakati ya Serikali kuiwezesha Takukuru na kuipa meno ya kuwashtaki moja kwa moja watuhumiwa wa rushwa.
Kambi hiyo imeilipua Taasisi ya Wanawake na Maendeleo (Wama) inayoongozwa na mke wa Rais, mama Salma Kikwete wakitaka ifutwe kwa maelezo kuwa imekiuka sheria za nchi.
Katika mjadala huo, Mbunge wa Muhambwe (NCCR-Mageuzi), Felix Mkosamali aliibua malumbano makali kati yake na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (Utawala Bora), George Mkuchika na Mwenyekiti wa Bunge, Lediana Mng’ong’o, baada ya kudai kuwa Ikulu na Serikali ya Awamu ya Nne imeshindwa kupambana na rushwa licha ya kuwa chini ya Rais.
Alivyochafua hali ya hewa
Katika mjadala huo, Mkosamali alihoji; “kama Takukuru, Mkurabita na Mfuko wa Maendeleo ya Jamii Tanzania (Tasaf) ziko chini ya Ofisi ya Rais na bado zinalia njaa, kwa nini watumishi wa umma kama wauguzi na walimu wawe chini ya ofisi hii badala ya kuwa katika Ofisi ya Waziri Mkuu au Tamisemi?
“Yaani njaa imeanzia Ikulu. Tumeiweka Takukuru Ikulu tukidhani kuwa Rais ataweza kupambana na rushwa, sasa ukiona taasisi hiyo imefeli tambua kuwa Rais hana utashi wa kisiasa wa kupambana na rushwa
“Watu wanajua Takukuru ikiwatuhumu katika kesi kubwa zitafutwa. Taasisi hii kufeli kufanya kazi maana yake ni kuwa Serikali imefeli katika miaka yote minane, hata Rais hakuwa na nia ya kupambana na rushwa,” alisema na kusisitiza jinsi Bunge la Katiba lilivyoshindwa kuipa meno Takukuru kupitia Katiba Inayopendekezwa.
Alihoji, “Tasaf wameomba Sh18 bilioni mwaka jana na mpaka sasa wamepewa Sh3 bilioni na sasa hivi mnaomba tena mabilioni ya shilingi. Hivi mnataka wakurugenzi wa Tasaf na wafanyakazi wawachukuliaje?”
Alihoji taasisi zilizopo chini ya Ofisi ya Rais kutopewa fedha za bajeti kama ilivyoidhinishwa mwaka jana na kusema kitendo cha mwaka huu wizara tatu za Ofisi ya Rais kuja na bajeti nyingine wakiomba mabilioni ya fedha ni fedheha.
“Kama taasisi zilizopo Ikulu zina njaa, hivi nyinyi huko katika halmashauri si ndiyo mtakufa! Rais ambaye taasisi hizi zipo ofisini kwake anashindwa kuzihudumia atawakumbuka watu wa Kibondo? Hii Serikali imechoka kabisa na imechakaa,” alisema.
Kauli hiyo ilimnyanyua Mkuchika na kuomba kutoa taarifa, jambo ambalo lilipingwa na Mkosamali akidai kuwa awali aliomba kutoa taarifa kwa mwenyekiti na kunyimwa.

mgomo wa Wanafunzi wa Chuo cha Ruaha Iringa leo MAY 20 2015

 

zachnews-news-update-logoMgomo wa wanafunzi wa Chuo Kikuu Dar ilikuwa ishu kubwa jana na pia ikapewa headlines kwenye Magazeti mengi ya leo May 20 2015.. ilianza kuzungumziwa mitandaoni hii ya leo mgomo mwingine Iringa, show ya XXL @CloudsFM ikampata mmoja wa wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Ruaha Iringa ambaye kasimulia hali iliyovyokuwa.
>>”Tunaishi katika hali ngumu tumeshindwa kuvumilia ikabidi tuchukue hatua za kufanya mgomo ili tupewe fedha zetu.. watu zaidi ya 100 wamekamatwa wengine wamepigwa.. tumepigwa mabomu ya machozi, watu wengine wapo Hospitali“>>
Mgomo ulianza chinichini kama siku nne zilizopita wakatuzima, ikaja barua kwamba Bodi haina hela.. hatukuwa na uhakika sana na hiyo barua ilionesha mwaka 2011 tulihisi imefojiwa.. Jana tukaanza kujipanga ili leo tufanye hii reaction.”>>—Mmoja wa wanafunzi hao.
Kamanda wa Polisi Iringa nae amepatikana na kuongelea ishu hiyo>>“Wanafunzi hawa jana walikutana usiku wamegawanyika kwenye makundi mawili, kuna kundi lilikuwa linahamasisha wenzao wagome ili waishinikize Serikali iwalipe mikopo yao.”>> Kamanda Mungi.
>>Jana walikutana kujadili njia gani waitumie kupata hiyo mikopo yao, baadhi yao walikubali wasubiri wataletewa hiyo mikopo wengine wakashinikiza kuwepo kwa hiyo migomo.. Asubuhi ya leo wengine walikuwepo darasani wengine wakataka kugoma.. Tukawa tunafatilia ambao walitaka kugoma wakawafanyia fujo wale ambao hawataki kugoma.>>
>>”Wakataka kutoka nje ya geti ili wakazuie barabara isipitike, tumewazuia kabla hawajatoka.. wamekamatwa wanafunzi 89.. tumepiga mabomu kama kuna mtu amepata mshtuko ni kwa mabomu lakini hakuna aliyejeruhiwa wala kuumizwa.>>
>>“Hali ni safi hakuna tatizo lolote.. kuna wanasiasa wameacha Bunge wamekuja huku, hatutaki mambo ya kisiasa yaingizwe kwenye mji wetu huu

Friday, 15 May 2015

OBAMA Talks Importance of Fathers, Faith at Catholic-Evangelical Summit on Overcoming Poverty



image: http://graphic.christianpost.com/images/new_article/ic_print.gif
image: http://graphic.christianpost.com/images/new_article/ic_print.gif
Sign Up for Free eNewsletter ››
BY NAPP NAZWORTH , CHRISTIAN POST REPORTER
May 12, 2015|5:15 pm
image: http://images.christianpost.com/full/83659/barack-obama.jpg
image: http://images.christianpost.com/full/83659/barack-obama.jpg
Barack Obama
image: 
image: 
(PHOTO: REUTERS/KEVIN LAMARQUE)
U.S. President Barack Obama takes part in the Catholic-Evangelical Leadership Summit on Overcoming Poverty at Georgetown University in Washington May 12, 2015.
WASHINGTON — President Barack Obama spoke Tuesday about the importance of faith and family during a panel discussion for the Catholic-Evangelical Summit on Overcoming Poverty at Georgetown University.
"Faith-based groups across the country and around the world understand the centrality and the importance of [poverty] in a intimate way — in part because these faith-based organizations are interacting with folks who are struggling and know how good these people are, and know their stories, and it's not just theological, but it's very concrete. They're embedded in communities and they're making a difference in all kinds of ways," Obama said.

Read more at http://www.christianpost.com/news/obama-talks-importance-of-fathers-faith-at-catholic-evangelical-summit-on-overcoming-poverty-139041/#qXBBwSB4lJdDLvxx.9
Obama also noted that he speaks about the importance of fathers to, for instance, students at Morehouse College, an all-male traditionally black college, more than Barnard College, an all-female college, because "I am a black man who grew up without a father and I know the cost that, I paid for that. And I also know that I have the capacity to break that cycle, and as a consequence, I think my daughters are better off."
Having that conversation, he added, "does not negate my conversation about the need for early childhood education, or the need for job training, or the need for greater investment in infrastructure, or jobs in low-income communities."
The summit was on its second of three full days of events. It was organized by Georgetown's Initiative on Catholic Social Thought and Public Life, and the National Association of Evangelicals. The goal of the summit is to "make overcoming poverty a moral imperative and urgent national priority." Partner groups participating in the event represent both conservative and liberal evangelical and Catholic groups.
Obama said he has read Putnam's new book, Our Kids: The American Dream in Crisis, which argues that a rich/poor opportunity gap has grown wider in recent years, such that poor kids find it more difficult to find success through hard work.
After Obama pointed out that anti-poverty programs have reduced poverty by 40 percent since 1967, Putnam noted that those programs have reduced poverty for the elderly but they have not helped children much.
Increasingly, he said, opportunities for success are determined by who your parents are. Poor children can be just as talented and hardworking, but their "fate is being determined by things that they had no control over, and that's fundamentally unfair."
Much of the discussion focused on areas where conservatives and liberals can find common ground.
Obama asked Brooks, the only conservative on the panel, if he would support increasing taxes on hedge fund managers to pay for early childhood education.
"If we can't ask society's lottery winners to just make that modest investment, then, really, this conversation is for show," Obama said.
Brooks answered that he does not speak for all Republicans but he would be fine with raising taxes on hedge fund managers. But doing so would not get at the main problem.
"Yes, sure. Fine," he said. "These are show issues. Corporate jets are show issues. Carried interest is a show issue. The real issue? Middle-class entitlements — 70 percent of the federal budget. That's where the real money is. And the truth of the matter is until we can take that on ... if the left and right want to make progress politically as they put together budgets, they're going to have to make progress on that."
Politicians cannot get to a conversation about spending that could help the poor, he continued, because they have not dealt with the entitlement issue.
"We can't even get to [a debate on anti-poverty programs] when politicians on the left and the right are conspiring to not touch middle-class entitlements. ... And when we're on an automatic path to spend tons of money in entitlements that are leading us to fiscal unsustainability, we can't get to these progressive conversations where conservatives and liberals ... work together, potentially, to help poor people," he said.

Read more at http://www.christianpost.com/news/obama-talks-importance-of-fathers-faith-at-catholic-evangelical-summit-on-overcoming-poverty-139041/#qXBBwSB4lJdDLvxx.99

Read more at http://www.christianpost.com/news/obama-talks-importance-of-fathers-faith-at-catholic-evangelical-summit-on-overcoming-poverty-139041/#bT71T2L3kXDlQw5F.99Having that conversation, he added, "does not negate my conversation about the need for early childhood education, or the need for job training, or the need for greater investment in infrastructure, or jobs in low-income communities."
The summit was on its second of three full days of events. It was organized by Georgetown's Initiative on Catholic Social Thought and Public Life, and the National Association of Evangelicals. The goal of the summit is to "make overcoming poverty a moral imperative and urgent national priority." Partner groups participating in the event represent both conservative and liberal evangelical and Catholic groups.
Obama said he has read Putnam's new book, Our Kids: The American Dream in Crisis, which argues that a rich/poor opportunity gap has grown wider in recent years, such that poor kids find it more difficult to find success through hard work.
After Obama pointed out that anti-poverty programs have reduced poverty by 40 percent since 1967, Putnam noted that those programs have reduced poverty for the elderly but they have not helped children much.
Increasingly, he said, opportunities for success are determined by who your parents are. Poor children can be just as talented and hardworking, but their "fate is being determined by things that they had no control over, and that's fundamentally unfair."
Much of the discussion focused on areas where conservatives and liberals can find common ground.
Obama asked Brooks, the only conservative on the panel, if he would support increasing taxes on hedge fund managers to pay for early childhood education.
"If we can't ask society's lottery winners to just make that modest investment, then, really, this conversation is for show," Obama said.
Brooks answered that he does not speak for all Republicans but he would be fine with raising taxes on hedge fund managers. But doing so would not get at the main problem.
"Yes, sure. Fine," he said. "These are show issues. Corporate jets are show issues. Carried interest is a show issue. The real issue? Middle-class entitlements — 70 percent of the federal budget. That's where the real money is. And the truth of the matter is until we can take that on ... if the left and right want to make progress politically as they put together budgets, they're going to have to make progress on that."
Politicians cannot get to a conversation about spending that could help the poor, he continued, because they have not dealt with the entitlement issue.
"We can't even get to [a debate on anti-poverty programs] when politicians on the left and the right are conspiring to not touch middle-class entitlements. ... And when we're on an automatic path to spend tons of money in entitlements that are leading us to fiscal unsustainability, we can't get to these progressive conversations where conservatives and liberals ... work together, potentially, to help poor people," he said.

Read more at http://www.christianpost.com/news/obama-talks-importance-of-fathers-faith-at-catholic-evangelical-summit-on-overcoming-poverty-139041/#qXBBwSB4lJdDLvxx.99

Read more at http://www.christianpost.com/news/obama-talks-importance-of-fathers-faith-at-catholic-evangelical-summit-on-overcoming-poverty-139041/#bT71T2L3kXDlQw5F.99